Skip to main content

Birdman, afunguka kuhusu kukosana na Lil wayne

Mwanzilishi wa Cash Money Records, Birdman amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusiana na kukosana na Lil Wayne ambaye alimshtaki na kumtaka amlipe dola milioni 51.

Pia kumekuwepo na tetesi kuwa Birdman alipanga kumuua Weezy baada ya basi lake la ziara kushambuliwa kwa bunduki. Birdman alizungumza kwa mara ya kwanza na mtangazaji wa Power 105. 1, Angie Martinez mjini Miami.

“Wayne ni mwanangu milele. Hicho hakitakuja kubadilika,” alisema.

“Nadhani kinachoendelea ni biashara tu na mtazamo wangu ni, nitafanya chochote anachotaka kufanya. Lakini atabaki kuwa mwanangu. Hakuna kitakachobadilisha ukweli kuwa [Lil Wayne] ni mwanangu. Mwisho wa siku, chochote anachotaka kufanya, nipo naye. Huyo ni mwanangu. Ninampenda hadi kufa. Ana baraka zangu na nitamsupport kwa lolote atakalochagua kufanya,” alisisitiza.

Birdman anasema bado anazungumza na Wayne na kwamba vyombo vya habari vinalikuza jambo hilo. Pamoja na kuheshimu mawazo yake, Birdman hayupo tayari kuacha Wayne aondoke kwenye label hiyo.

“Siwezi kumwacha aende, lakini kama anataka kwenda ntaheshimu matakwa yake,” alisema. “Akisema anataka kwenda, siwezi kumzuia. Akiniambia ‘baba ni muda wa kwenda,’.. sijasikia kutoka kwenye mdomo wake.”

Birdman amekanusha pia kumrushia pombe Wayne alipokuwa akitumbuiza kwenye klabu hivi karibuni. “Siwezi mwenyewe kumtupia kitu mtoto wangu.”

Kuhusu madai kuwa yeye na Young Thug walipanga kumuua Lil Wayne, Birdman alisema, “Hicho pengine ni kitu cha kijinga kabisa kuwahi kukisikia katika maisha yangu.”

Kuhusu kutakiwa amlipe Weezy dola milioni 51, Birdman alisema, “Sihisi kama ananidai dola milioni 50. Nilimpa mkataba wa zaidi ya dola milioni 100 na advance ya $60-70 million.”

Katika hatua nyingine Birdman alisema Nicki Minaj na Drake hawawezi kuondoka Cash Money.

Popular posts from this blog

MAPENZI NI NINI?: Jua maana ya mapenzi

SOCIAL HALL    Upendo umetokana na neno la kigiriki “ahab aheb” lenye maana hisia kali na muhathirika wa ndani. Upendo ni hisia kali, upendo chimbuko lake ni moyoni upendo ni Mungu ameuweka ndani ya moyo wa mwanadamu, upendo ni maisha ya mtu na ni utaratibu wa mtu hivyo mtu anapo amua kumpenda mtu mwingine mtu huyu anakua ameamua kuhatarisha maisha yake kwa mtu Fulani. Ameamua kuuweka moyo wake kwa mtu Fulani. Ameathirika ndani ya moyo wake kwa ajili ya mtu Fulani akili ambayo ndio chanzo cha mapenzi imekubaliana nayo. Najua kuwa unajua kuwa mapenzi ni akili,kama akili ikichoka hakuna mapenzi hivyo ndio maana hata maandiko yanasema “ Ishini na wake zenu kwa akili”   Maana mapenzi la kweli yanahitaji akili timamu uwe na muda wa kufikiri kabla ujafanya lolote. Kuishi na mtu kunahitaji akili timamu, sasa mtu huyu amefanya maamuzi ya kiakili, kimwili na kiroho kuwa wewe unamfaa hivyo unatakiwa kuyaheshimu...

Historia ya Lil wayne

Lil Wayne Lil Wayne mnamo 2011 Maelezo ya awaliAmezaliwa 27 Septemba   1982 (umri 34)Asili yake New Orleans, Louisiana ,  United States Aina ya muziki Hip hop Kazi yake Rapa ,  Mwigizaji ,  CEO ,  Msanifu [1] Ala Sauti Miaka ya kazi1993–mpaka sasa Studio Cash Money ,  Young Money ,  Universal Ame/Wameshirikiana na Hot Boys ,  Birdman ,  T-Pain ,  Drake ,  Young Money ,  Kanye West ,  Young Jeezy ,  DJ Khaled ,  Mack Maine ,  Rick Ross Tovuti www.lilwayne-online.com Dwayne Michael Carter, Jr.  (amezaliwa tar.  27 Septemba   1982 ) ni mshindi wa  Tuzo za Grammy  - akiwa kama rapa wa muziki wa hip hop bora kutoka nchini  Marekani . Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama  Lil Wayne . Alijiunga na studio ya  Cash Money Records  akiwa bado yungali bwana mdogo na akabahatika kufanya rekodi kadhaa katika studio hiyo. Wayne alikuwa mmoja kati ya waliokuwa ...

Freemason na familia 13 za Illuminant

FREEMASONS NA FAMILIA 13 ZA ILUMINATI NI chama cha Prieure de Sion (Priory de Sion) kilichoanzishwa na familia ya 11 ya Illuminati inayoitwa Freeman Illuminati bloodlines ndicho kilichosababisha kuanzishwa kwa ‘Uprotestant’ au ‘Upinzani’ ndani ya dini. Wakainuka mashujaa wengi waliopinga mafundisho machafu yaliyoingizwa ndani ya imani ya kweli ili kutetea neno la Mungu litawale tofauti na mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Miongoni mwa mashujaa walioinuka kupingana na mafundisho ya chama cha Prieure de Sion alikuwa Martin Luther. Kumbuka kwamba wapinzani ‘Protestants’hawa walikuwa wanapinga mafundisho wakiwa ndani ya mifumo ya dini zao. Hata hivyo hawakufanikiwa kuleta matokeo mazuri ya upinzani wao na hivyo wakaamua kutoka na kujitenga na dini wakiwa na baadhi ya mafundisho machafu waliyoyarithi kutoka kwenye mifumo potofu ya kidini. Wakiwa wamejitenga, sasa waliamua kufanya ‘matengenezo’ kwa lengo la kuondoa mafundisho machafu na ku...