Skip to main content

Hakuna utajiri wa shorcut kwenye mitandao, Piga jazi Kijana

Kuna baadhi ya watu hasa vijana ambao wamekuwa wao kutwa kucha ni kuhangaika kwenye mitandao, ‘INTANETI’ wakitafuta njia ama mitandao wanayodai ni ya kuwaunganisha na taasisi au vyama vitakavyowasaidia kupata utajiri wa haraka au haramu. Wanapokutana na tovuti kama hizi za kwetu zilizokuwa na majina au kaulimbiu zenye hisia za utajiri au pesa,  basi pasipo hata kusoma makala hizo kama ndani zinazungumzia kitu gani wao moja kwa moja huhisi wameshakutana na kile walichokuwa wakikitafuta, mara moja huanza kupiga simu wakiulizia jinsi ya kujiunga na mtandao wanaodhani unagawa utajiri.

Mgunduzi wa INTANETI Sir Tim Berners Lee hapo mwaka 1989.

Tunapenda kuwashauri na kuwaeleza ukweli kwamba, kwanza mtandao wa Intaneti watu waliouasisi akiwemo mgunduzi mwenyewe Sir Berners Lee mwaka 1989, hata na akina Steve Jobs mgunduzi wa kompyuta hizi za mezani tunazotumia leo miaka ya 70 pamoja na smart phones, Bilionea Bill Gates mzee wa software aliyeanza tangu miaka hiyo ya 70 pamoja na ‘Bwanamdogo’ Mark Zurkerberg aliyeasisi FACE BOOK juzijuzi mwaka 2004, wote hawa  hawakuwa na lengo la intaneti itumike kwa malengo haramu au ya kuleta uharibifu, intaneti ililetwa kumkomboa binadamu, kumpa uhuru ikiwa ni pamoja na kuwaondolea wanyonge hali ya kutokuwa na haki ya kupata taarifa na kuondokana na minyororo ya umasikini.

Mwanzilishi  wa kampuni ya Apple komputa za mezani, na smartphones, Hayati Steve job.

Uliwahi kusikia skendo za akiina Edward Snoden na Julian Assange wa Wikileaks, na Marekani taifa kubwa lilipotaka kuutumia mtandao wa intaneti na teknolojia ya habari kukandamiza haki za watu wakawaida, uliona ilivyopigiwa kelele na wanateknolojia, wagunduzi wenyewe na wapenda haki duniani? Hivyo nataka utambue jinsi ambavyo intaneti isivyopaswa kutumiwa kwa maswala ambayo hayana maadili wala kumjali binadamu wa kawaida. Tena waasisi hao waliofanya kazi ngumu usiku na mchana wakivuja jasho ili kuvumbua teknolojia ya kumkomboa mwanadamu wangekusikia ukisema unataka utumie intaneti kwa malengo hasi ya kutaka kutajirika kimiujiza pasipo kufanya kazi wangekushangaa sana.


Mwanzilishi wa mtandao maarufu wa facebook Mark Zuck.

Uchawi, nguvu za giza, dhana potofu, chuki, uvunjivu wa haki za binadamu, kueneza hofu, wizi, unyanganyi, ulaghai, uwongo, ama ubaguzi wa aina yeyote ule wa binadamu iwe ni kikabila, dini au rangi hauna nafasi kabisa kwenye mtandao wa intaneti. Kama huamini haya ninayoyasema ukidhani intaneti ni kichaka cha wahalifu au watenda maovu basi hebu anzisha blogu, au website yeyote ile kisha uanze kuhubiri chuki, au mambo ambayo yanaingilia uhuru wa watu wengine tuone kama utakaa hewani hata miezi 2.

Julian Assange kushoto na Edward Snowden kulia. 

Kwa hiyo ukisikia kuna mtandao au tovuti inayoweza kumpa mtu utajiri kwa njia za kimiujiza usikubali, kataa, hizo ni “scams” utapeli. Utajiri unakuja baada ya mtu kufanya kazi halali akizingatia kanuni zote za ujasiriamali na wala hakuna utajiri unaoweza kupatikana ndani ya kipindi kifupi kama mwezi mmoja miwili au hata mwaka, labda iwe umeshinda bahati na sibu au umerithi mali za wazazi wako baada ya Mungu kuwachukua. Unaweza kutajirika kwa kuweka malengo na mipango ya muda mfupi na mrefu. Kitabu cha MIFEREJI 7 YA PESA NA SIRI MATAJIRI WASIYOPENDA KUITOA kimeelezea vizuri sana namna unavyoweza ukajiwekea malengo yako ya kiuchumi na kimaisha kwa ujumla.

- See more at: http://www.jifunzeujasiriamali.com/utajiriwamiujiza.html#sthash.2DiTNG4k.dpuf

Popular posts from this blog

MAPENZI NI NINI?: Jua maana ya mapenzi

SOCIAL HALL    Upendo umetokana na neno la kigiriki “ahab aheb” lenye maana hisia kali na muhathirika wa ndani. Upendo ni hisia kali, upendo chimbuko lake ni moyoni upendo ni Mungu ameuweka ndani ya moyo wa mwanadamu, upendo ni maisha ya mtu na ni utaratibu wa mtu hivyo mtu anapo amua kumpenda mtu mwingine mtu huyu anakua ameamua kuhatarisha maisha yake kwa mtu Fulani. Ameamua kuuweka moyo wake kwa mtu Fulani. Ameathirika ndani ya moyo wake kwa ajili ya mtu Fulani akili ambayo ndio chanzo cha mapenzi imekubaliana nayo. Najua kuwa unajua kuwa mapenzi ni akili,kama akili ikichoka hakuna mapenzi hivyo ndio maana hata maandiko yanasema “ Ishini na wake zenu kwa akili”   Maana mapenzi la kweli yanahitaji akili timamu uwe na muda wa kufikiri kabla ujafanya lolote. Kuishi na mtu kunahitaji akili timamu, sasa mtu huyu amefanya maamuzi ya kiakili, kimwili na kiroho kuwa wewe unamfaa hivyo unatakiwa kuyaheshimu...

Historia ya Lil wayne

Lil Wayne Lil Wayne mnamo 2011 Maelezo ya awaliAmezaliwa 27 Septemba   1982 (umri 34)Asili yake New Orleans, Louisiana ,  United States Aina ya muziki Hip hop Kazi yake Rapa ,  Mwigizaji ,  CEO ,  Msanifu [1] Ala Sauti Miaka ya kazi1993–mpaka sasa Studio Cash Money ,  Young Money ,  Universal Ame/Wameshirikiana na Hot Boys ,  Birdman ,  T-Pain ,  Drake ,  Young Money ,  Kanye West ,  Young Jeezy ,  DJ Khaled ,  Mack Maine ,  Rick Ross Tovuti www.lilwayne-online.com Dwayne Michael Carter, Jr.  (amezaliwa tar.  27 Septemba   1982 ) ni mshindi wa  Tuzo za Grammy  - akiwa kama rapa wa muziki wa hip hop bora kutoka nchini  Marekani . Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama  Lil Wayne . Alijiunga na studio ya  Cash Money Records  akiwa bado yungali bwana mdogo na akabahatika kufanya rekodi kadhaa katika studio hiyo. Wayne alikuwa mmoja kati ya waliokuwa ...

Freemason na familia 13 za Illuminant

FREEMASONS NA FAMILIA 13 ZA ILUMINATI NI chama cha Prieure de Sion (Priory de Sion) kilichoanzishwa na familia ya 11 ya Illuminati inayoitwa Freeman Illuminati bloodlines ndicho kilichosababisha kuanzishwa kwa ‘Uprotestant’ au ‘Upinzani’ ndani ya dini. Wakainuka mashujaa wengi waliopinga mafundisho machafu yaliyoingizwa ndani ya imani ya kweli ili kutetea neno la Mungu litawale tofauti na mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Miongoni mwa mashujaa walioinuka kupingana na mafundisho ya chama cha Prieure de Sion alikuwa Martin Luther. Kumbuka kwamba wapinzani ‘Protestants’hawa walikuwa wanapinga mafundisho wakiwa ndani ya mifumo ya dini zao. Hata hivyo hawakufanikiwa kuleta matokeo mazuri ya upinzani wao na hivyo wakaamua kutoka na kujitenga na dini wakiwa na baadhi ya mafundisho machafu waliyoyarithi kutoka kwenye mifumo potofu ya kidini. Wakiwa wamejitenga, sasa waliamua kufanya ‘matengenezo’ kwa lengo la kuondoa mafundisho machafu na ku...