Skip to main content

Vitu usivyovijua kuhusu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam

Mkuu wa mkoa Dar es salaam Paul Makonda.Na. Dorcas Safiel, Alex Sonna.

Hii ni historia ya muheshimiwa paul makonda mkuu wa mkoa jijini Dar es salaam, amezaliwa tarehe 15\2\1982 huko Kolomije wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza katika zahanati ya Kolomije siku ya Jumatatu saa 1;30 Asubuhi ni mtoto wa kipekee wa kiume katika familia ya mzee Makonda na bi.Suzan
mh.Paul Makonda ametoka kwenye familia ya kawaida mama yake alisoma mpaka darasa la 7 na baba yake hakusoma kabisa lakini pia alihishi katika kusudi la mungu na kumtumikia pia ni kitu kilichomfanya awe bora katika ukuaji wake wakati wote, alibahatika kuwa na ndugu  wa kike lakini aliweza kuishi ndani ya mwaka na nusu toka kuzaliwa kwake na kufariki dunia. 

Amesoma shule ya msingi katika shule ya kolomije,sekondari alisoma kutokana na changamoto za kipato katika familia hakuweza kwenda kidato cha tano na kwenda chuo Mbegani chuo cha uvuvi mjini bagamoyo kuanza ngazi ya cheti,diploma na ata kufika chuo kikuu katika kuchukua shahada yake sifa kubwa aliyokuwa nayo chuoni na aliyoacha hapo  wanafunzi wengi kubadilika tabia na kumtumikia mungu, Pia nyumbani alikuwa mchapakazi asiye mvivu alikuwa radhi kukaa njaa lakini kufanya kazi daima hasa katika kulima alimpa mama yake faraja pale alipokuwa na huzuni, lakini msikivu kwa kila mtu amekuwa faraja katika familia ya makonda wakati wote katika maisha yake hakuwayi kufikiri kama kuna mtu atamfanyia mahamuzi zaidi yake mwenyewe. Mh.Paul Makonda ametia maisha magumu ili tu aweze kupata shahada moja alikuwa utingo wa kubeba mizigo ya watu huko mkoani Mwanza,mwaka 2001-2002 alikuwa mchimba mchanga na mkata mkaa huko Mbezi Luis pia amewayi kuwa waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi Muccobs.
Mh. Paul Makonda akiwa katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015
Ni mwana siasa kupitia chama cha mapinduzi( CCM) kabla ya kuwa mkuu wa wilaya aliwayi kuwa katibu wa umoja wa vijana wa ccm( uvccm) uhamasishaji na chipukizi, wakati wa Rais mstaafu dkt.Jakaya Mrisho Kikwete aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya mkoani Dar es salaam mnamo tarehe 18|2|2015 jambo ambalo alifurahi sana na kwenda kumshukuru Mungu, changamoto ambazo aliwayi kupitia ni kama zifuatazo.
 changamoto ya muda kwake ilikuwa ni kubwa sana kwani alitamani yawe masaa48 ili aweze kufanya kazi zake vizuri.changamoto ya migogoro ya ardhi ambayo ilimpelekea kutoa 75% kuwalipa wanasheria kwa ajili ya kutatua migogoro hiyo.ufisadi uliokithirirushwauchafu wa mazingira wilaya ya kinondonihuduma za afya na elimu.Hata hivyo tarehe 13\3\2016 Rais wa muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuri aliweza kumteuwa kuwa mkuu wa mkoa wa jiji la Dar es salaam katika sekta ya kuwa mkuu wa mkoa alikuta changamoto zifuatazo;
omba omba jijini Dar es salaam ambao walikuwa chanzo cha uchafu wa jiji na kufanyika kwa uharifu na kushuka kwa elimu.madawati shuleniupungufu wa shule za sekondari za serikali.uchafu uliokithiri jijini Dar es salaam wasichana wanao jiuza miili yao.utumiaji mbaya wa sehemu za starehe.Mh,Paul makonda kwanza ni kijana mdogo katika siasa na pia mkakamavu kwani mtu yeyote anaweza kujifunza kupitia kwake kuhusu maisha lakini pia haya ni mambo 8 usiyo yajua juu ya Mh.Paul Makonda katika kupenda kazi yake pamoja na nchi yake ya Tanzania..

28\2\2016 Mkuu wa wilaya ya kinondoni Paul Makonda aliaza kupiga hatua ya kuwapigania walimu ili waweze kusafiri bure ikiwa kama jukumu lake la kusaidia kutekeleza lengo la Rais dkt.John Pombe Magufuri kuboresha sekta ya elimu. 16\2\2016 Mh.Paul Makonda aliaza mkakati wa kukabiliana na tatizo la ajira katika wilaya yake kwa kuanzisha mashindano ya vijana kwa jina la kinondoni talent search .8\3\2016 Aliazisha mkakati wa maalum wa kuanzisha mtaa maalum utakaokuwa ukihusika na biashara ya vinywaji vikali na baridi kama bar. 20\3\2016 Alitoa rai kwa watu wanaotumia silaha kinyume na sheria kwenda kuzisalimisha katika kituo cha polisi lakini hakuishia hapo aliahidi kutoa kitika cha shilingi million moja kwa yule atakayetii agizo hilo na kuahidi kutochukuliwa hatua yeyote.10\5\2016 Katika sakata la sukari nchini Tanzania alikuwa kiongozi mnzuri wa kukamata tani 4 za sukari zilizofichwa wilaya ya kinondoni.9\5\2016Katika suala la kutumbua majipu ya watumishi hewa seikalini bado alikuwa vinzuri kwa kumsimamisha Afisa utumishi wa wilaya ya ilala baada ya kushindwa kubaini wafanyakazi hewa 11 waliokuwa wilaya hiyo. 11\4\2016 mkakati wa kuanza kupamba na omba omba kando ya barabara jijini dar uliaza April 18\4\2016 ambao waliotolewa katika maeneo ya barabara ili kupumguza uhalifu,na kufanya waweze kurudi makwao kujishughulisha.

30\4\2016 Alizindua kampeni ya usafi mkoani Dar es salaam iliyofanyika katika viwanja vya Leaders Clubs na kauli mbiu ilikuwa "usijifanye mstaarabu kuwa mstaarabu" kwa lengo la kuboresha hali ya usafi katika mitaa mbali mbali pamoja na jiji la Dar es salaam kwa ujumla.Hayo ni baadhi kati ya mengi aliyoyafanya Mh.Paul Makonda katika jiji la Dar es salaam akionyesha kukubali kufanya yote ambayo ni kero jijini hapa ndani ya miaka 5 na mengine mengi ambayo yapo njiani kuja. 

Popular posts from this blog

MAPENZI NI NINI?: Jua maana ya mapenzi

SOCIAL HALL    Upendo umetokana na neno la kigiriki “ahab aheb” lenye maana hisia kali na muhathirika wa ndani. Upendo ni hisia kali, upendo chimbuko lake ni moyoni upendo ni Mungu ameuweka ndani ya moyo wa mwanadamu, upendo ni maisha ya mtu na ni utaratibu wa mtu hivyo mtu anapo amua kumpenda mtu mwingine mtu huyu anakua ameamua kuhatarisha maisha yake kwa mtu Fulani. Ameamua kuuweka moyo wake kwa mtu Fulani. Ameathirika ndani ya moyo wake kwa ajili ya mtu Fulani akili ambayo ndio chanzo cha mapenzi imekubaliana nayo. Najua kuwa unajua kuwa mapenzi ni akili,kama akili ikichoka hakuna mapenzi hivyo ndio maana hata maandiko yanasema “ Ishini na wake zenu kwa akili”   Maana mapenzi la kweli yanahitaji akili timamu uwe na muda wa kufikiri kabla ujafanya lolote. Kuishi na mtu kunahitaji akili timamu, sasa mtu huyu amefanya maamuzi ya kiakili, kimwili na kiroho kuwa wewe unamfaa hivyo unatakiwa kuyaheshimu...

Historia ya Lil wayne

Lil Wayne Lil Wayne mnamo 2011 Maelezo ya awaliAmezaliwa 27 Septemba   1982 (umri 34)Asili yake New Orleans, Louisiana ,  United States Aina ya muziki Hip hop Kazi yake Rapa ,  Mwigizaji ,  CEO ,  Msanifu [1] Ala Sauti Miaka ya kazi1993–mpaka sasa Studio Cash Money ,  Young Money ,  Universal Ame/Wameshirikiana na Hot Boys ,  Birdman ,  T-Pain ,  Drake ,  Young Money ,  Kanye West ,  Young Jeezy ,  DJ Khaled ,  Mack Maine ,  Rick Ross Tovuti www.lilwayne-online.com Dwayne Michael Carter, Jr.  (amezaliwa tar.  27 Septemba   1982 ) ni mshindi wa  Tuzo za Grammy  - akiwa kama rapa wa muziki wa hip hop bora kutoka nchini  Marekani . Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama  Lil Wayne . Alijiunga na studio ya  Cash Money Records  akiwa bado yungali bwana mdogo na akabahatika kufanya rekodi kadhaa katika studio hiyo. Wayne alikuwa mmoja kati ya waliokuwa ...

Freemason na familia 13 za Illuminant

FREEMASONS NA FAMILIA 13 ZA ILUMINATI NI chama cha Prieure de Sion (Priory de Sion) kilichoanzishwa na familia ya 11 ya Illuminati inayoitwa Freeman Illuminati bloodlines ndicho kilichosababisha kuanzishwa kwa ‘Uprotestant’ au ‘Upinzani’ ndani ya dini. Wakainuka mashujaa wengi waliopinga mafundisho machafu yaliyoingizwa ndani ya imani ya kweli ili kutetea neno la Mungu litawale tofauti na mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Miongoni mwa mashujaa walioinuka kupingana na mafundisho ya chama cha Prieure de Sion alikuwa Martin Luther. Kumbuka kwamba wapinzani ‘Protestants’hawa walikuwa wanapinga mafundisho wakiwa ndani ya mifumo ya dini zao. Hata hivyo hawakufanikiwa kuleta matokeo mazuri ya upinzani wao na hivyo wakaamua kutoka na kujitenga na dini wakiwa na baadhi ya mafundisho machafu waliyoyarithi kutoka kwenye mifumo potofu ya kidini. Wakiwa wamejitenga, sasa waliamua kufanya ‘matengenezo’ kwa lengo la kuondoa mafundisho machafu na ku...