Skip to main content

Posts

Ngono ni kipimo cha huba

Wanaume wengi wanatumia kigezo hiki kama kuthibitisha au kudhihirisha mapenzi ya dhati. Utamsikia mwingine anasema: “Sasa kama hutaki kufanya mapenzi na mimi, utakuwa hunipendi.” Kwa sababu wanawake nao wanaogopa kuachwa au wanatamani ndoa, kwa kuamini kwamba tendo hilo ni kila kitu wanajikuta wakikubali; sasa hapo inategemea, mwisho unaweza kuwa mzuri au mbaya! MAPENZI NI NINI HASA? Kila mmoja anaweza kuwa na maana yake, lakini kimsingi mapenzi hayana maana ya moja kwa moja! Kwa ujumla mapenzi ni hisia zenye msisimko wa pendo la dhati zinazotoka moyoni mwa mmoja kwenda kwa mwingine. Pendo hukamilika ikiwa wawili hao kwa wakati mmoja watahisi hisia hizo, ingawa wakati mwingine mmoja ndiyo huwa wa kwanza kuanza kuhisi hisia hizo. Tafsiri hii nimewahi kuitaja mara kadhaa katika makala zangu, kama wewe ni mdau wa kona hii utakuwa unakumbuka, kama ndiyo kwanza unasoma hapa, basi si vibaya maana utakuwa umeingiza kitu kichwani mwako. Wakati mwingine inawezekana mkajikuta mm...
Recent posts

MAPENZI NI NINI?: Jua maana ya mapenzi

SOCIAL HALL    Upendo umetokana na neno la kigiriki “ahab aheb” lenye maana hisia kali na muhathirika wa ndani. Upendo ni hisia kali, upendo chimbuko lake ni moyoni upendo ni Mungu ameuweka ndani ya moyo wa mwanadamu, upendo ni maisha ya mtu na ni utaratibu wa mtu hivyo mtu anapo amua kumpenda mtu mwingine mtu huyu anakua ameamua kuhatarisha maisha yake kwa mtu Fulani. Ameamua kuuweka moyo wake kwa mtu Fulani. Ameathirika ndani ya moyo wake kwa ajili ya mtu Fulani akili ambayo ndio chanzo cha mapenzi imekubaliana nayo. Najua kuwa unajua kuwa mapenzi ni akili,kama akili ikichoka hakuna mapenzi hivyo ndio maana hata maandiko yanasema “ Ishini na wake zenu kwa akili”   Maana mapenzi la kweli yanahitaji akili timamu uwe na muda wa kufikiri kabla ujafanya lolote. Kuishi na mtu kunahitaji akili timamu, sasa mtu huyu amefanya maamuzi ya kiakili, kimwili na kiroho kuwa wewe unamfaa hivyo unatakiwa kuyaheshimu...

Saikolojia: Namna ya kutambua tabia ya mtu

Hakuna anayependa kusahihishwa, kugombana au kukemewa mbele za watu, hii ndiyo tabia ya watu wajeuri na walio na tabia za kitukutu. Mara nyingine hudhani wanapata sifa. Wako watu wa jinsi hii ambao hawawezi kukugombeza au (kukupa vidonge vyako) mkiwa wawili peke yenu, watangoja watu wengine wawepo ndiyo waanze kubwabwaja, cha kufanya jiepushe nao. Kwa kule kukimbiwa na marafiki, na kuwa mpweke, huongeza tabia za kitukutu na kijeuri na hii huwafanya watu hawa kutambulika haraka na kiurahisi zaidi. Zifuatazo ni alama zitakazokutambulisha mtu jeuri na mtukutu: a) Alama za kimaneno Mara kwa mara hupendelea kusema maneno haya vinywani mwao. Nakwambia bora unge…" Wewe sichochote, silolote…" Nakwambia, lazima u..." Fanya vile ninavyokuambia mimi…" Nataka u..." Wewe endelea tu tutaona..." b) Alama za kimwili Hupendelea kusimama wima Huwa wenye pozi kavu, ngumu (still and rigid pause) Hupenda kukunja mikono Hupenda kupay...

Vitu usivyovijua kuhusu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam

Mkuu wa mkoa Dar es salaam Paul Makonda. Na. Dorcas Safiel, Alex Sonna . Hii ni historia ya muheshimiwa paul makonda mkuu wa mkoa jijini Dar es salaam, amezaliwa tarehe 15\2\1982 huko Kolomije wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza katika zahanati ya Kolomije siku ya Jumatatu saa 1;30 Asubuhi ni mtoto wa kipekee wa kiume katika familia ya mzee Makonda na bi.Suzan mh.Paul Makonda ametoka kwenye familia ya kawaida mama yake alisoma mpaka darasa la 7 na baba yake hakusoma kabisa lakini pia alihishi katika kusudi la mungu na kumtumikia pia ni kitu kilichomfanya awe bora katika ukuaji wake wakati wote, alibahatika kuwa na ndugu  wa kike lakini aliweza kuishi ndani ya mwaka na nusu toka kuzaliwa kwake na kufariki dunia.  Amesoma shule ya msingi katika shule ya kolomije,sekondari alisoma kutokana na changamoto za kipato katika familia hakuweza kwenda kidato cha tano na kwenda chuo Mbegani chuo cha uvuvi mjini bagamoyo kuanza ngazi ya cheti,diploma na ata kufika chuo kikuu katika kuchuk...

Hakuna utajiri wa shorcut kwenye mitandao, Piga jazi Kijana

Kuna baadhi ya watu hasa vijana ambao wamekuwa wao kutwa kucha ni kuhangaika kwenye mitandao, ‘INTANETI’ wakitafuta njia ama mitandao wanayodai ni ya kuwaunganisha na taasisi au vyama vitakavyowasaidia kupata utajiri wa haraka au haramu. Wanapokutana na tovuti kama hizi za kwetu zilizokuwa na majina au kaulimbiu zenye hisia za utajiri au pesa,  basi pasipo hata kusoma makala hizo kama ndani zinazungumzia kitu gani wao moja kwa moja huhisi wameshakutana na kile walichokuwa wakikitafuta, mara moja huanza kupiga simu wakiulizia jinsi ya kujiunga na mtandao wanaodhani  unagawa utajiri . Mgunduzi wa INTANETI Sir Tim Berners Lee hapo mwaka 1989. Tunapenda kuwashauri na kuwaeleza ukweli kwamba, kwanza mtandao wa Intaneti watu waliouasisi akiwemo mgunduzi mwenyewe  Sir Berners Lee mwaka 1989 , hata na akina Steve Jobs mgunduzi wa kompyuta hizi za mezani tunazotumia leo miaka ya 70 pamoja na smart phones, Bilionea Bill Gates mzee wa software aliyeanza tangu miaka hi...

JINSI UNAVYOWEZA KUWEKEZA KATIKA MFUMO WA BIASHARA YA MTANDAO NA KUBADILI MAISHA YAKO BADAE

  Mtaji mkubwa wa Biashara ya Mtandao sio pesa, mtaji mkubwa ni jinsi ya kujua kutumia muda wako vizuri, jitihada pamoja na mtaji watu ambao wanakuzunguka ujue jinsi ya kuwashirikisha.    Hapa nakushirikisha baadhi ya  hatua mhimu nilizotumia mimi kuchagua ni kampuni gani inanifaa kufanya nayo biashara ili niweze kufikia malengo yangu, na hivi ndio vigezo mhimu vya kuzingatia. Jinsi ya kuanza biashara ya Mtandao(Network marketing) *HATUA YA KWANZA. Kwanza ifahamu maana ya Biashara ya mtandao. Kuna tofauti ya neno mtandao linalotumika hapa katika biashara hii mpya na neno “mtandao” kama linavyotumika katika upande wa mawasiliano. Katika Biashara ya Mtandao (Network Marketing), neno mtandao linamanisha “jumuia, timu au kikundi cha watu ambacho kimeungana na kinaendelea kupanuka kwa idadi ya watu kuongezeka kwa lengo la kila mtu aliopo katika timu na anayejiunga  kumiliki biashara yake kama wakala wa kujitegemea katika kampuni husika. ...

Jinsi ya kupata likes nyingi facebook

Watumiaji wengi wa facebook wamekuwa wakitamani kupata LIKES  nyingi kwenye status na picha zao wanazo post facebook lakini wameshindwa . Leo nitatoa hatua chache za kufuata ili nawe uweze kuwa miongoni mwa wanaopata LIKE nyingi facebook STEP 1: Download Application Ya MG LIKES => Download MG-LIKERS Hapa STEP 2: Install hiyo app uliyo idownload kisha uifungue STEP 3: Bonyeza login (with facebook STEP 4: Ingiza human verification Security Captcha STEP 5: Bonyeza (Get likes now click here to see your post) STEP 6: Bonyeza (Feed Likes) STEP 7: Chagua post unayotaka kuiongezea Likes halafu ubonyeze "Submit Mwisho utaambiwa LIKES DONE NB: Unaweza kuomba Likes kila baada ya dakika kumi na tano, na kiwango cha juu ni Likes 200 kwa kila unapoomba